Kuna aina kadhaa za mifumo ya tathmini ambayo inatumiwa kulingana na
mahitaji au mazingira ya sehemu husika.mifumo hiyo ni kama vile;ufatiliaji wa
Matumizi ya fedha za umma(public expenditure system and survey),ushirikishwaji
wa jamii ya vijiji katika tathmini(participatory rural appraisal(PRA),tathmini
ya uwajibikaji wa jamii(social accountability monitoring)na PIMA KADI
Mifumo yote hiyo imeainishwa utaratibu ambao unaweza kutumika katika
kukusanya taarifa inayokusudiwa katika kuijenga jamii uwezo,kuiwezesha kuwa na
kauli na kushiriki ipasavyo katika kutathimini na kuiwajibisha mamlaka husika
pale inapobainika kuwa rasilimali za umma zimetumika kinyume na jinsi ilivyokusudiwa.Mifumo yote
hiyo ni sahihi na inafaa kutumika kilingana na chaguo la sehemu husika.
Katika muongozo huu ,mfumo mkuu wa tathmini utakaotumika na
tutakaojikita nao zaidi ni mfumo wa ufatiliaji wa matumizi ya fedha za umma au
PETS,pia tutaangalia kwa undani kuhusu zana ya PIMA KADI na jinsi inavyotumika
kama nyenzo ya kukusanya taarifa.
Kwa ujumla PETS na mifumo yake imesaidia kujibu maswali ambayo mara
nyingi wananchi wamekuwa wanajiuliza ili kupima tathimini ya fedha zilizopangwa
au kutumika na matokeo husika .Hivyo kupitia PETS wananchi wanaweza kufanya
tathimini na kupata ufumbuzi wa maswali yanayowakabili kuhusu mgawanyo wa
matumizi ya rasilimali zao. Baadhi ya maswali ambayo wananchi hujiuliza ni kama
yafuatayo
1)je,fedha na rasilimali za umma huwafikia wananchi hususani wale wa
ngazi ya chini mfano wanawake na watoto kama ilivyokusudiwa ?
2)je,rasilimali fedha na rasilimali zingine zinawafikia wananchi kwenye
maeneo husika kwa mtizamo wa kijinsia?
Utaona kuwa swali la kwanza linalohoji mtiririko wa fedha na rasilimali
za umma zitolewazo ama na serikali kuu au wafadhili au wabia wa kimaendeleo ili
kugharamia miradi ya maendeleo katika kijiji,kata.Mantiki yake ni kutaka
kufahamu ni kiasi gani cha fedha na rasilimali za umma zimewafikia walengwa au
watoa huduma,kama vile hospitali,shule ,maji ,barabara nk kama ilivyokusudiwa.
Katika kufanya tathmini na kujiuliza maswali hayo ,na iwapo kuhoji huko
kunaweza kukasababisha uchunguzi na ikadhihirika kuwepo na utofauti ya fedha
zilizotolewa katika ngazi ya serikali kuu na kiasi kilichopelekwa kwa watoa
huduma katika ngazi za nchini,huo unaitwa uvujaji.Hii inamaanisha kuwa baadhi
ya pesa au rasilimali zilizotolewa kwa ajili ya miradi ya
maendeleo,hazijatumika kulingana na sera au maleng yaliyokusudiwa na serikali
au mamlaka husika.maana yake ni kuwa fedha au rasilimali hizi zimekwapuliwa
katika ngazi Fulani ya kiutawala,inaweza kuwa wilayani au mikoani.
Hali kadhalika ,swali la pili linalenga zaidi katika uchambuzi.Lengo ni
kubainisha kwa nini uvujaji hujitokeza.Mara nyingi,hujibu maswali kama vile
,kwa nini uvujaji hutokea katika baadhi ya halmashauri zaidi ya zingine?Au kwa
nini shule ,halmashauri kadhaa hupokea fedha na rasilimali nyingi kuliko
zingine
Kwa kufanya utambuzi huo ,mfumo unawezesha namna ya kufatilia ili
kupunguza uvujaji na kuboresha utendaji na uwajibikaji katika ngazi ya
ki-serikali /uongozi /utawala husika
Hivyo basi,ili kuondosha mianya ya rushwa na kuimarisha utawala bora
katika ngazi zote husika za uongozi,ni vyema kutambua mianya ya rushwa,ambapo
suala la kuwajengea uwezo wananchi au wapokeaji wa huduma,litaweza kusaidia
usimamizi na udhibiti wa rasilimali katika maeneo yote.Pia kwa kutumia mfumo wa
PETs wananchi watadai taarifa za matumizi kulingana na huduma zitolewazo ,pia
watahoji kiwango cha utendaji kazi wanapokuwa na shaka ,hivyo kuzuia kushamiri
kwa rushwa kwa viongozi wao.