Ni hari isiyotegemewa na kila mtu katika mazingira yetu ,katika eneo moja lilipo BUZA maeneo ya kituo cha mama kibonge alimaarufu kama kwa dona limezua kasheshe baada ya eneo hilo kugawiwa kwa wananchi kwa ajili ya kufanya biashara ndogondogo,awali kabla maeneo haya jatolewa uongozi huo uliwatangazia watu kwa ajili ya kuandikisha majina na namba zao za simu ili waweze kuwagawia kwa utararatibu,wananchi zaidi ya 3000 waliitikia wito na kujiandikisha lakini baada ya muda kidogo utaratibu ukabadilika wakatangaza wanagawa maeneo bila kuita majina bali wanampatia mtu yeyote mwenye biashara hapo hapo jambo ili liliwakwaza baadhi ya watu walio andika majina.
Tathimini inaonyesha asilimia kubwa ya wafanya biashara hao ni wanachama
mbalimbali wa VIKOBA baada ya kuwahoji asilimia kubwa ya watu walinithibitishia
wao wapo katika VIKOBA .Tangu niingie
vikoba sijawahi kuangaika kama jinsi nilivyokuwa katika mikopo ya saccos,benk
na hata pride lakini sasa nina raha sana katika kikundi kikoba hivyo lazima nijishughulishe ili nipate
fedha ya marejesho ya hisa kila wiki,ni mama Faudhia alifunguka kwa furaha
jinsi VIKOBA inavyo mpa raha
Eneo ni kubwa linavyoonekana litahusisha michezo mbalimbali ya watoto
mfano bembea,treni la umeme,na vitu vingi ambavyo wananchi walisikia kama
fununu.
Mategemeo
yetu eneo hili liwe kubwa kama Tandika sokoni ili nasi tuweze fanya biashara
tujipatie kipato,tunamshukuru aliyejitolea kutupa maeneo kiukweli ameona mbali
sana hatuna cha kumlipa ila Mungu ndo atamlipa.ni Aisha
Mbeya mwanachama wa VIKOBA mkazi wa kata ya makangarawe aliongea maneno hayo
kwa upole sana
Maeneo haya yanasemekana ni ya kanisa la Angrikana ,wanahabari wetu
walijaribu kumtafuta kiongozi wa kanisa hakupatikana .