Translate

Translate

Wednesday, 19 March 2014

JE?KWA NINI SERIKALI NYINGI ZA MTAA HAZINA UBAO WA MATANGAZO KWA NJE?cheki picha katika blog

Tunapozungumzia serikali ya mtaa(local government)ni wazi kabisa wengi tunatambua tuna zungumzia serikali gani,kwa asilimia kubwa nchini serikali hii ipo kila mtaa kwa ajili ya wananchi wake na wala si kwa ajili ya viongozi wa serikalini lakini cha ajabu zaidi ni kwamba asilimia ya wananchi wengi wanaogopa kuwa karibu na serikali yao ambayo ipo kwa ajili yao wenyewe.
Mbao za matangazo aziwekwi kwa sababu ni sehemu ambayo wananchi ni rahisi kupata taarifa na kuhoji endapo taarifa sio sahii na mara nyingi taarifa zinakuwa na kasoro za kiubadhirifu.
Kuna vitu muhimu sana vya kuzingatia kama wananchi wa Tanzania hasa kwa ajili ya maendeleo yetu wenyewe kasumba kubwa ni kwamba tumenyimwa elimu ya kuelewa vitu vya msingi ili tuweze nyanyaswa pasipo na hatia,mara nyingi viongozi wa mtaa wakichaguliwa wanabadilika sana tunawanajiona tofauti na wananchi wa kawaida.
Sheria inatambua kabisa haki na wajibu wa mwananchi na viongozi,mwananchi anayo haki ya kuuliza na kuhoji swala la maendeleo katika mtaa wake pasipo kuvunja sheria ya nchi
KUMBUKA SERIKALI YA MTAA YOYOTE LAZIMA IWE NA UBAO WA MATANGAZO AMBAO UNAONYESHA MAPATO NA MATUMIZI NA TAARIFA ZINGINE MUHIMU.

Hivyo kama mwanajamii na haki yako kuuliza na kuhoji ni muhimu sana kufatilia ili kujiletea maendeleo sisi wenyewe lazima tuanze chini alafu ndo tupande juu.

No comments: