Mwananchi ana wajibu na majukumu yake kuhakikisha kuwa kiongozi
aliyemchagua au kuteuliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo katika viwango
vinavyokubalika katika eneo la kijiji/mtaa.Kila mwananchi ana wajibu wa kupanga
na kukataa kila aina ya uovu katika jamii ikiwemo rushwa,uonevu,wizi,ubadhilifu
wa mali za umma nay a watu binafsi.
Mwananchi pia wana jukumu la kudai na kupigania haki zao za wananchi
wengine kutoa malalamiko na kuuliza maswalijuu ya mambo mbalimbali vya jamii na
kiserikali.Wananchi wanashiriki katika serikali za mitaa kupitia vikao au
mikutano mbalimbali ambapo hujadili na kutoa mapendekezo yao kuhusu mipango na
matatizo yanayowakabili kwa namna moja au nyingine ili kuweza kupatiwa ufumbuzi
na kurahisiha uboreshaji wa huduma za kijamii katika maeneo yao wanamoishi.
VIZURI SOMO LA DEMOKRASIA TUNGEIPIGANIA MPAKA VIONGOZI WAIFATE IPASVYO
No comments:
Post a Comment