Kwa kuwa,
sisi wananchi wa jamhuri wa muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati
kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya
utu,uhuru,haki,usawa,udugu,amani,umoja na mshikamano katika Nyanja zote za
maisha yetu;
Na
kwa kuwa,tunaamini kuwa misingi hiyo inaweza tu kutekelezwa
katika jamii yenye mfumo wa kidemokrasia na utawala bora ambayo serikali yake
inasimamiwa na Bunge lenye Wabunge waliochaguliwa na wanaowakilisha wananchi,na
Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo
kudumisha na kwamba wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu
Na kwakuwa ,tunatambua
umuhimu wa kutunza mali ya mamlaka ya nchi na pamoja,kupiga vita aina zote za
uharibifu,ubadhirifu na kuhimiza matumizi bora na endelevu ya rasilimali na
mustakabali wa maisha ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo;
Na
kwa kuwa,tunatambua umuhimu na faida za kujenga,kukuza na
kuendeleza amani,umoja,urafiki na ushirikianao
miungoni mwa watanzania,mataifa mbalimbali ya Afrika na duniani kwa
ujumla;
Na kwa
kuwa,azma ya kujenga umoja wa bara la Afrika
inadhihirishwa na Muungano wa iliyokuwa jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya
watu Zanzibar;
Na kwa kuendeleza dhamira yetu hiyo,ni muhimu:
a)kulinda,kuimarisha na kuudumisha muungano wa nch za jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya
watu wa Zanzibar;
b)kujenga Taifa huru na linalojitegemea;
c)kuimarisha na kuendeleza utawala wa sheria;
d)kukuza na kuendeleza maadili,uwajibikaji na uwazi;
e)kujenga umoja na mshikamano utakaowezesha kutimiza
malengo ya kisiasa,kiuchumi ,kijamii,kimazingira na kulinda urithi kwa ujumla;
f)kujenga na kuendeleza ukuu wa mamlaka ya watu;
g)kujenga na kuendeleza utii wa mamlaka ya katiba;na
h)kuimarisha na kudumisha uzalendo kwa taifa miungoni
mwa watanzania;
NA
KWA KUZINGATIA,urithi tulioachiwa wa waasisi wa Taifa letu wa
kujenga nchi yenye umoja wa watu wake ambao hawabaguani kwa misingi ya
ukabila,dini ,rangi,jinsi au ubaguzi wa aina nyingine yoyote;
NA
KUZINGATIA,uzoefu wa zaidi ya miaka hamsini ya uhuru wa
Tanganyika,miaka hamsini ya mapinduzi ya Zanzibar na miaka hamsini ya muungano
wa jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya watu wa Zanzibar,na uhumuhimu wa
ushiriki mpana na bayana wa wananchi katika utungaji wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania;
HIVYO
BASI,KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE
MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI WANACHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WATANZANIA
kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni
ya kujenga jamii kama hiyo,na kuhakikisha kuwa jamhuri ya muungano wa Tanzania
inaongozwa na serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na utawala wa
sheria,kujitegemea na isiyofungamana na dini.
TOA MAONI YAKO
No comments:
Post a Comment