TASAF MTAA WA MAKANGARAWE TEMEKE
WAZUA MASWALI MENGI
Mpango wa
serikali wa kunusuru kaya maskini awamu ya tatu (TASAF) ukiwa katika
utekelezaji wake wa kuhakikisha wanawafikia walengwa wa mradi huo ambao kaya
maskini umepelekea kuwemo kwa maswali mengi ya msingi kutoka kwa baadhi
ya wananchi walio hudhuria kikao hicho mtaa Makangarawe,Kata ya Makangarawe, Wilaya Temeke Dar es salaam.
Akizungumza katika mkutano mwenyekiti wa mtaa Juma Mohamed Kibanda alisema"Mpango huu wa TASAF ni mpango wa kunusuru kaya maskini ambao kwa sasa umetufika wanamakangarawe hivyo tushirikiane katika kufikia lengo na kuwafikia walengwa"aliendelea kusema "Mpango huu ni wamendeleo hasa katika kaya maskini ". Akizungumza mwezeshaji wa TASAF ambae alielezea malengo
na faida za mpango huo wa TASAF. Jambo ambalo lilizua maswali
mengi na hoja za msingi kutoka kwa wanajamii wa Makangarawe ili
kujilidhisha kama mpango huo ni waukweli au ni jambo la kisiasa ambalo linaleta
mkanganyiko kutokana na ukaribu wa uchaguzi jambo ambalo lishawahi kujitokeza
mwaka 2005 .
No comments:
Post a Comment