Translate

Translate

Friday, 2 January 2015

SOMA UFAHAMU KWA KINA JUU YA KAMATI ZA SERIKALI ZINAVYOKWENDA KINYUME NA SHERIA ZA NCHI kwa faida yetu sote

KAMATI  ZA HALMASHAURI YA KIJIJI/KAMATI YA MTAA

Ø Kuna kamati tatu za halmashauri ya kijiji/mtaa kisheria
Ø Kamati ya fedha,mipango na uchumi ,huduma za jamii na shughuli za kujitegemea na ulinzi na usalama
Ø Mkutano mkuu wa kijiji/mkutano wa wakazi wa mtaa una uwezo wa kuagiza halmashauri ya kijij/kamati ya mtaa kuundaa kamati ya muda kwa shughuli maalum au halmashauri yenyewe inaweza kuunda kukiwa na haja ya kufanya hivyo.
Ø Idadi ya wajumbe katika kamati inashauriwa wasipungue wajumbe watatu 3 na wasizidi wajumbe watano 5
Ø Kamati za kisheria inafaa ziongozwe na mjumbe wa halmashauri ya kijiji /kamati y mtaa
Ø Inashauriwa wenyekiti wa kijiji /mtaa , wenyeviti wa vitongoji  wasiwe wenyeviti wa kamati mbalimbali ili kutolimbikiza madaraka yote kwa halmashauri ya kijiji/kamati ya mtaa
Ø Wananchi  wakaida wanaweza kuwa wajumbe wa kamati au wanaweza kuitwa kutoa ushauri kwenye vikao vya kamati
Ø  Kamati zinaweza kukutana mara kwa mara kutunza kumbukumbu na kuendesha vikao kwa kushauriwa na afisa mtendaji wa kijiji (VEO)/ Afisa mtendaji wa mtaa(MEO)

No comments: