Ndugu
mkurugezi wa baraza la dini mbalimbali za dini Tanzania;
Ndugu
washirika wa maendeleo,
Ndugu maafisa wa serikali,
Ndugu
wawakilishi wa mashirika ya kiraia,
Ndugu
wawakilishi kutoka kamati za PETS vijijini,
Ndugu
wanahabari,
Wageni
waalikwa,
Mabibi na
mabwana.
Ndugu
mkulugenzi;
Awali ya yote napenda nitumie nafasi hii kwanza kumshukuru
mwenyezi Mungu ,kwa kutupa uzima,afya,nguvu ,na kibali cha kutuwezesha kukutana
katika tukio hili muhimu .Nilishukuru pia baraza la dini mbalimbali nchini kwa
kuhakikisha tukio hili muhimu linafanyika ili tuweze kuzungumzia masuala
mbalimbali muhimu kuhusu mstabali wa maendeleo ya wananchi .Nashukuru pia kwa
maamuzi yenu ya kuialika TAMISEMI katika shughuli hii kwani kwa kweli sisi ndio
wenye dhamana kubwa na shughuli mbalimbali zinzzomlenga mwananchi wa kawaida
.Ndio maana pamoja na majukumu tuliyo nayo BUNGENI kwa sasa lakini baada ya
kupata mwaliko wenu tumefanya maamuzi ya kuweza kushiriki.Niwape pole pia
washiriki mbalimbali waliotoka nje ya Dar es salaam kwa safari ndefu kutoka sehemu
mbalimbali kuja hapa kushiriki kongamano hili muhimi.
Ndugu
washiriki,
Napenda pia kutambua mchango na kutoa shukrani za dhati kwa
wadau mbalimbali wamaendeleo na Taasisi mbalimbali kwa kuwezesha maandalizi ya
shughuli hii kufanyika wakiwemo Baraza kuu la waislam Tanzania
(BAKWATA,)jumuiya ya wakristo Tanzania(CCT),Baraza kuu la maaskofu
katoliki Tanzania (TEC),Kanisa la
kiinjili la kilutheli Tanzania ,shirika la kikristu linalotoa huduma kwa
wakimbizi Tanganyika(TCRS),Shirika la shughuli za maendeleo ya wanawake
(WIA)pamoja na shirika la maendeleo la Norway(NCA).Mchango wenu ni mkubwa sana
katika kusukuma gurudumu la MAENDELEO kwa wananchi na kwa Taifs kiujumla
,ninatambua kuwa na ushirka wa madhehebu ya dini katika kuchangia maendeleo
nchini ni wa kihistoria.Ninapenda kuwapongeza zaidi kwa kuwa sasa sit u
mnatukumbusha kuwajibika kupitia ibada mbalimbali bali pia mnashiriki katika
kuelimisha jamii hata nje ya nyumba za ibada.Lakini kwa namna ya pekee zaidi
napenda kuwapongeza kwa kuwa tunapata fursa ya kutafakari juu ya wajibu wetu katika kuleta maendeleo
endelevu.
Ndugu
Mkurugenzi na Washiriki,
Mandeleo ya nchi yanawezekana endapo kila mmoja wetu mahali
alipo atatizama wajibu wake kwa malengo na bila kusukumwa. Malengo ndio msingi
mkubwa katika utendaji kazi.Kwa watumishi wa umma,pamoja na malengo mengine
lengo kuu ni kuhakikisha kuwa wanawatumikia wananchi kwa kadri ya uwezo
,kujituma na kuwa waaminifu na wabunifu katika kutumia rasilimali zilizopo kwa
ufanisi.Sote tunafahamu kuwa hakuna siku ambayo mtu atasema rasilimali zilizopo
zinamtosheleza.lakini ni imani yangu kwamba,rasilimali ndogo zilizopo
zikitumika vema zinaweza kuleta mabadiliko katika undendaji na baadae kuleta
maaendeleo makubwa ya Taifa na wananchi kwa ujumla .Tangu kupata uhuru,serikali
imekuwa ikifanya jitihada kuhusu kuhakikisha kuwa huduma bora zinawafikia
wananchi.katika kufanikisha jambo hili,serikali imekuwa ikichukuwa hatua
mbalimbali ikiwemo kuanzishwa kwa mpango wa uboreshaji wa serikali za mitaa
ulioanza mwaka1998 ambao unalenga katika kupeleka madaraka kwa wananchi.Lengo
la kuwa na maboresho ni kuhakikisha kuwa mamlaka za serikali za mitaa zinapewa
uhuru wa kufanya maamuzi mbalimbali yahusuyo utoaji wa huduma kwa wananchi na
kuwakilisha wananchi katika kujiletea Maendeleo na ustawi wao kwa ujumla.
Ndugu
Mkurugenzi na Washiriki,
Kwa mujibu wa sharia ya serikali za mitaa sura ya
287,majukumu ya mamlaka za serikalia za mitaa ni pamoja na kudumisha
amani,usalama ,utulivu na kutoa huduma bora za jamii na kiuchumi kwa wananchi
,kutekeleza shughuli za maendeleo pamoja na kupanga mipango ya maendeleo endelevu.Aidha ,serikali inazingatia sana
suala la ushirikishwaji wa wananchi katika mipango mbalimbali na utekelezaji wa
wananchi katika mipango mbalimbali na utekelezaji wa shughuli za maendeleo.Hili
linafanyika kwa kuzingatia Mpango wa fursa na vikwazo kwa Maendeleo
(opportunities and obstacles to Development-O&OD).Mpango huu ulianzishwa na
serikali sambamba na awamu ya pili ya program ya maboresho ya serikali za Mitaa(2002)kwa
lengo la kusaidia jamii kuwa na uelewa mkubwa kuhusiana na umiliki wa
mchakato wa maendeleo.Maelekezo
ya kuwashirikisha wananchi katika shughuli za maendeleo ni ya lazima na
maendeleo,sharia za fedha na hata katiba ya nchi.
Ndugu
Mkurugenzi na washiriki,
Dhana na lengo la kuwa
na ufuatiliaji wa Matumizi ya Rasilimali za Umma kwa wananchi ni suala muhimu
katika kuhakikisha rasilimali za Nchi zinatumika ipasavyo na hatimaye kuboresha
huduma za jamii. Sote tunafahamu panapotokea kufujwa,kuharibiwa au kupotea kwa
rasilimali za umma ambazo zilipangwa katika kuendeleza utoaji wa huduma kwa
wananchi ,watu wote huathirika bila kujali dini,kabila rangi au eneo.Hivyo basi
ili kuwa na uhakika wa matumizi mazuri ya rasilimali hizo,wananchi wote bila kujali
tofauti zao za kiimani,hawana budi kuungana na kushirikiana pamoja katika
ufuatiliaji wa mapato ya matumizi ya rasilimali zao. Serikali inatambua na kuthamini jitahada zinazofanywa na umoja wenu katika
kutekeleza miradi ya kuijenga uwezo jamii kushiriki kufuatilia mapato na
matumizi ya rasilimali za Umma katika wilaya takribani 25 Tanzania bara na
visiwani.Nakiri kuwa yapo mafanikio kutokana na baadhi ya viongozi wasiowajibika katika kuwa mafunzo yenu yamewezesha kwa kiasi kikubwa kujenga
uwajibikaji na kuboresha utolewaji wa taarifa na huduma katika maeneo
mbalimbali.Azma ya serikali ni kuendelea kutoa ushirikiano nanyi wakati wote.
Ndugu
Mkurugenzi na Washiriki,
Napenda nitumie fursa hii kutoa wito kwenu na jamii kwa jumla
kuendelea kutoa ushirikiano kwa kuwabaini baadhi ya viongozi wa Halmashauri na
vijiji wasio waaminifu wanaochangia kurudisha nyumba juhudi za kuleta maendeleo
kwa kujinufaisha binafsi.Wapo viongozi
waliopewa dhamana ya kusimamia rasilimali za umma ikiwepo fedha za uendeshaji
wa shule,huduma ya afya na pembejeo za kilimo lakini hawazifikishi katika
maeneo husika.Ninapenda kuwatia moyo wanakamati za PETS pamoja na jamii kwa
jumla kutokana tama pale wanapoona viongozi wachache wasio waadilifu wanatumia
vibaya madaraka yao kujinufaisha binafsi. Jambo la msingi ni kuzingatia kuwa
Nchi yetu inaongozwa kwa msingi ya sheria na Utawala bora. Hivyo tuepuke
kujichukulia sheria mkononi au kufanya maamuzi yanayopaswa kuamuliwa kisheria.Tumieni vyombo vinavyohusika na
wahamasisheni wananchi kuzingatia sheria
za Nchi
pale yanapojitokeza mapungufu kwa watendaji wa serikali na kwa jamii kwa
ujumla.Vipo vyombo kama vile Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa –TAKUKURU
na Jeshi la polisi,vitumieni ili
watuhumiwa washughulikiwe kwa mujibu wa sheria.Viongozi wa vijiji na
Halmashauri zote nchini wanao wajibu wa
kutoa ushirikiano wa dhati na wakati wote milango yetu ipo wazi kwa ajili ya
kupokea ushauri na maoni yenu.
Ndugu
washiriki,
Mwisho napenda kuwasisitiza juu ya umuhimu wa kuendelea na
kuhamasisha umoja wa Taifa letu hasa katika kipindi hiki ambacho baadhi ya watu
wameanza kupandikiza hisia za udini kwa wananchi kwa malengo binafsi.Nchi hii
ni yetu sote na wote tunawajibika kuuenzi mshikamano ambao tumekuwa nao katika kipindi chote tangu tulipopata
uhuru. Umoja na Amani tulivyonavyo ni
msingi ambayo waasisi wa Taifa hili wametuachia kama urithi wa pekee
kabisa.Navikikosekana vitu hivi dhana nzima ya maendeleo kwa wananchi wetu
itakuwa ni ndoto. Ninafahamu wote
tunatambua changamoto zilizotokea katika nchi za jirani na jinsi ambavyo watoto
na kina mama wasio na hatia walivyoathirika na wengine kupoteza maisha.Naomba
wote kwa pamoja tuwe walinzi wa Amani na Utulivu tulio nao. Vitu hivi
vikitoweka sisi sote bila kujali DINI,KABILA NA RANGI zetu tutapata madhara
makubwa sana.
Nimalize kwa kuwatakia Mdahalo wenye mafanikio katika kukuza
uwezo wa wananchi kufuatilia Matumizi ya Rasilimali za Umma kwa kuleta
maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.
Baada ya kusema haya machache napenda nitamke kuwa kongamano
hili limefunguliwa rasmi.
ASANTE
SANA