Translate

Translate

Monday, 1 December 2014

TUJITAZAME KISHA TUTAZAME NA WENGINE

SIKU ZOTE KAZI NZURI UONGOZI MZURI, KATIKA SWALA LA UWAZI NA UWAJIBIKAJI UANZIE KWETU KWANZA NDO TWENDE KUHAMASISHA WENGINE KAMA MIONGONI MWA KAZI AMBAZO ZINA FANYWA NA TAASISI AU ASASI AU DINI FULANI ALAFU NDANI YAKE HAKUNA UKWELI NA UWAZI WA KUNYAMBULISHA MAMBO NI WAZI KABISA TUTAKUWA TUNATWANGA MAJI KWENYE KINU LAZIMA KATIKA KUFANYA KAZI NZURI YENYE MAFANIKIO LAZIMA UONGOZI NA WATU WAKE WASHIRIKIANE PAMOJA KATIKA KUPANGA MIKAKATI MAHUSUSI YA KUFIKIA LENGO KAMA KUTAKUWA NA MIZUNGUKO KATIKA KUTOA MAELEZO SAHII HILO NI TATIZO NA HATUWEZI TATUA MATATIZO MENGINE, JAMBO HILI NI LAKUZINGATIA SANA , UNAWEZA UKAWA NA MOYO WA KUJITOLEA KATIKA KAZI FULANI KWA LENGO ZURI LAKINI UNAPONYIMWA HAKI YAKO UNAKATISHWA TAMAA YA KUENDELEA NA KAZI HIVYO BASI MABADILIKO YAANZIE KWETU NDO TUPELEKE KWA WENGINE USIMAMIZI MBOVU KAZI MBOVU DAIMA.

Sunday, 2 November 2014

HALI HALISI YA MBAGALA BUS TERMINAL KATIKA WILAYA YA TEMEKE

Makala
leo asubuhi nikiwa katika safari zangu nimekerwa sana na hili la mbagala bus terminal nadhani hata wewe kama mwananchi wa mbagala unalijua hilo na linakukela pia
kwa wale ndugu zangu mliofika mbagala bus terminal mnajua hali halisi katika stand hiyo ya mabasi makubwa na madogo , ni wazi kabisa serikali inatambua kama ni wajibu wao katika uboreshaji , lakini tunasema uwajibikaji na utawala bora ni kasumba nzito sana nchi

katika  kuuliza uliza kwangu inasemekana kila basi linaloingia pale linalipa ushuru kwa ajili ya stand bila shaka hata wafanyabiashara pale wanalipa ushuru wa eneo la stand yamkini hata wewe ni mmoja wapo katika sehemu fulani unalipa kodi au ushuru wa serikali , lakini kama wananchi tunahaki ya kujua fedha hizo tunazo katwa ni kwa ajili ya matumizi yapi. Mbagala inatambulika kila sehemu nje na ndani ya nchi kibiashara na hata kimapato ya nchi

kwenu wahusika wakuu katika uboreshaji wa mazingira ya mbagala bus terminal ni wazi mnapata mapato yetu lakini hamtaki kuyafanyia kazi iweje terminal kubwa kama mbagala bado inavumbi chini mpangilio mbovu wa magari hata mazingira ya usafi hakuna uduma za choo hazilidhishi?

Watanzania wenzangu bila kusimama wenyewe hatuta weza kusimamishwa sisi ndo watu wa kufanya mabadiko tuachane na mambo ya umimi tuungane kuweza kujiwekea mazingira salama wenyewe kwani uwezi mkuta mtoto wa viongozi wa kiwa katika mazingara ambayo tunayaishi sisi.
Tusisubiri kusukumwa tuanze wenyewe.




Saturday, 1 November 2014

NIMELUDI SASA

Ni baada ya kupotea kidogo ili kuweka sawa mambo fulani kwa lengo la kuboresha kazi nzuri zaidi
sasa unatakiwa kuwa taayari na kufatilia blog yangu ili kuweza kupata taarifa zinazo kuhusu wewe
kama mdau wa jamii kiujumla .
Pia nachukuwa nafasi hii kuwatakaradhi watu wangu waliokuwa wanafatilia blog hii
kwa kuwanyima taarifa zinazo wahusu sasa endelea kujifunza zaidi.
ASANTE

Saturday, 26 April 2014

MKUKUTA NI NINI?soma ujilidhishe

MKUKUTA ni nini?NI kifupisho cha maneno ya Kiswahili yenye maana ya mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini Tanzania.
MKUKUTA awamu ya 1(2005/06-2009/10)ulilenga katika kukuza uchumi ,kupunguza umasikini wa kipato ,ubora wa maisha ya watu na ustawi wa jamii pamoja na kuimarisha utawala bora na uwajibikaji .utekelezaji wake ulienda sambamba na uandaaji wa ripoti za kila mwaka zikiainisha uzoefu ,mafanikio na changamoto.
Kila mwaka ripoti zilijadiliwa na wadau mbalimbali katika makongamano na mikutano ya kitaifa ya sera.Maoni kutoka kwenye mapitio na mijadala hiyo yalitumika katika kuboresha mpango wa mwaka uliofuata.
MKUKUTA inachangia katika utekelezaji wa dira ya taifa ya maendeleo(2025)na malengo ya maendeleo ya millennia (2015).

Tuesday, 15 April 2014

SOMA UJUE VYANZO VYA HAKI VYA MWANANCHI WA TANZANIA

HAKI ZA UHALALI WA MWANANCHI KUFATILIA MATUMIZI YA RASILIMALI ZA UMMA(PETS)
Haki ni stahili ya binadam .Hii inamaanisha kuwa mtu ana haki kwa kuwa anastahili ya kutenda jambo Fulani,au wengine wanatakiwa kutenda au kumtendea jambo Fulani katika hali Fulani . Haki zinaweza kuwa binafsi au za jumla . Kwa lugha rahisi ,tunasema kuwa haki ni stahili za msingi ambazo binadamu yeyote Yule bila kujali jinsia ,umri ,itikadi,dini,rangi ,kabila au aina yoyote ya utofauti huzaliwa nazo na hazitolewi na mtu na wala haziwezi kuondolewa na mtu kwa sababu yeyote .vivyo hivyo ,uhalali wa mtu kufanyanya au kufanyiwa jambo Fulani ,unatikana na stahili ambayo mtu au wattu wanakuwa nayo kw mujibu wa sheria ,sera kanuni ,taratibu au muongozo husika,Ni kwa muktadha huo,wananchi kupitia sheria ,sera,matamko ,mikataba ,kanunui na miongozo mbalimbali ,wanapata haki na uhalali wa kufuatilia matumizi ya rasilimali za umma kila mara wanapoona inafaa kufanya hivyo

                 NB;VYANZO VYA HAKI
a)mila na desturi
b)katiba ya nchi
c)sera na miongozo
c)sheria za nchi
d)kanuni na mikataba ya kitaifa /kimataifa

Saturday, 12 April 2014

MIFUMO YA TATHIMINI NA UFATILIAJI WA RASILIMALI ZA UMMA(PETS)

Kuna aina kadhaa za mifumo ya tathmini ambayo inatumiwa kulingana na mahitaji au mazingira ya sehemu husika.mifumo hiyo ni kama vile;ufatiliaji wa Matumizi ya fedha za umma(public expenditure system and survey),ushirikishwaji wa jamii ya vijiji katika tathmini(participatory rural appraisal(PRA),tathmini ya uwajibikaji wa jamii(social accountability monitoring)na PIMA KADI
Mifumo yote hiyo imeainishwa utaratibu ambao unaweza kutumika katika kukusanya taarifa inayokusudiwa katika kuijenga jamii uwezo,kuiwezesha kuwa na kauli na kushiriki ipasavyo katika kutathimini na kuiwajibisha mamlaka husika pale inapobainika kuwa rasilimali za umma zimetumika  kinyume na jinsi ilivyokusudiwa.Mifumo yote hiyo ni sahihi na inafaa kutumika kilingana na chaguo la sehemu husika.
Katika muongozo huu ,mfumo mkuu wa tathmini utakaotumika na tutakaojikita nao zaidi ni mfumo wa ufatiliaji wa matumizi ya fedha za umma au PETS,pia tutaangalia kwa undani kuhusu zana ya PIMA KADI na jinsi inavyotumika kama nyenzo ya kukusanya taarifa.
Kwa ujumla PETS na mifumo yake imesaidia kujibu maswali ambayo mara nyingi wananchi wamekuwa wanajiuliza ili kupima tathimini ya fedha zilizopangwa au kutumika na matokeo husika .Hivyo kupitia PETS wananchi wanaweza kufanya tathimini na kupata ufumbuzi wa maswali yanayowakabili kuhusu mgawanyo wa matumizi ya rasilimali zao. Baadhi ya maswali ambayo wananchi hujiuliza ni kama yafuatayo
1)je,fedha na rasilimali za umma huwafikia wananchi hususani wale wa ngazi ya chini mfano wanawake na watoto kama ilivyokusudiwa ?
2)je,rasilimali fedha na rasilimali zingine zinawafikia wananchi kwenye maeneo husika kwa mtizamo wa kijinsia?
Utaona kuwa swali la kwanza linalohoji mtiririko wa fedha na rasilimali za umma zitolewazo ama na serikali kuu au wafadhili au wabia wa kimaendeleo ili kugharamia miradi ya maendeleo katika kijiji,kata.Mantiki yake ni kutaka kufahamu ni kiasi gani cha fedha na rasilimali za umma zimewafikia walengwa au watoa huduma,kama vile hospitali,shule ,maji ,barabara  nk kama ilivyokusudiwa.
Katika kufanya tathmini na kujiuliza maswali hayo ,na iwapo kuhoji huko kunaweza kukasababisha uchunguzi na ikadhihirika kuwepo na utofauti ya fedha zilizotolewa katika ngazi ya serikali kuu na kiasi kilichopelekwa kwa watoa huduma katika ngazi za nchini,huo unaitwa uvujaji.Hii inamaanisha kuwa baadhi ya pesa au rasilimali zilizotolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo,hazijatumika kulingana na sera au maleng yaliyokusudiwa na serikali au mamlaka husika.maana yake ni kuwa fedha au rasilimali hizi zimekwapuliwa katika ngazi Fulani ya kiutawala,inaweza kuwa wilayani au mikoani.
Hali kadhalika ,swali la pili linalenga zaidi katika uchambuzi.Lengo ni kubainisha kwa nini uvujaji hujitokeza.Mara nyingi,hujibu maswali kama vile ,kwa nini uvujaji hutokea katika baadhi ya halmashauri zaidi ya zingine?Au kwa nini shule ,halmashauri kadhaa hupokea fedha na rasilimali nyingi kuliko zingine
Kwa kufanya utambuzi huo ,mfumo unawezesha namna ya kufatilia ili kupunguza uvujaji na kuboresha utendaji na uwajibikaji katika ngazi ya ki-serikali /uongozi /utawala husika
Hivyo basi,ili kuondosha mianya ya rushwa na kuimarisha utawala bora katika ngazi zote husika za uongozi,ni vyema kutambua mianya ya rushwa,ambapo suala la kuwajengea uwezo wananchi au wapokeaji wa huduma,litaweza kusaidia usimamizi na udhibiti wa rasilimali katika maeneo yote.Pia kwa kutumia mfumo wa PETs wananchi watadai taarifa za matumizi kulingana na huduma zitolewazo ,pia watahoji kiwango cha utendaji kazi wanapokuwa na shaka ,hivyo kuzuia kushamiri kwa rushwa kwa viongozi wao.

Wednesday, 9 April 2014

UTAWALA WA KIDEMOKRASIA KATIKA JAMII NINI?soma ufahamu.

Mwananchi ana wajibu na majukumu yake kuhakikisha kuwa kiongozi aliyemchagua au kuteuliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo katika viwango vinavyokubalika katika eneo la kijiji/mtaa.Kila mwananchi ana wajibu wa kupanga na kukataa kila aina ya uovu katika jamii ikiwemo rushwa,uonevu,wizi,ubadhilifu wa mali za umma nay a watu binafsi.
Mwananchi pia wana jukumu la kudai na kupigania haki zao za wananchi wengine kutoa malalamiko na kuuliza maswalijuu ya mambo mbalimbali vya jamii na kiserikali.Wananchi wanashiriki katika serikali za mitaa kupitia vikao au mikutano mbalimbali ambapo hujadili na kutoa mapendekezo yao kuhusu mipango na matatizo yanayowakabili kwa namna moja au nyingine ili kuweza kupatiwa ufumbuzi na kurahisiha uboreshaji wa huduma za kijamii katika maeneo yao wanamoishi.



TUNGEIJUA 
VIZURI SOMO LA DEMOKRASIA TUNGEIPIGANIA MPAKA VIONGOZI WAIFATE IPASVYO

Monday, 7 April 2014

SAFISHA JIJI TANDIKA SOKONI WAKIMBIZANA NA MIZIGO tazama picha


Operesheni ya safisha jiji katika mji wa dar es salaam umekuwa gumzo kubwa sana katika maeneo mbalimbali jijini dar es salaam baada ya wafanyabiashara kukimbizana na mizigo yao ili kuepusha shari ya serikali,
katika eneo la Tandika sokoni jana asubuhi wafanyabiashara hao ambao waliweka biashara zao katika maeneo yasiyo sahihi walikumbwa na operesheni hiyo ya kusafisha jiji,pia katika maeneo ya mbagala safisha jiji ilifanyika kupitia jeshi la polisi likisaidiaana na jeshi la wagambo.


Friday, 4 April 2014

JE? NI KWELI JAMHURI YA MUUNGANO INAENZI NA KUZINGATIA TUNU HIZI soma uzijue tunu za Taifa

JAMHURI YA MUUNGANO ITAENZI NA KUZINGATIA TUNU ZA TAIFA ZIFUATAVYO:
a)utu;
b)azalendo;
c)uadilifu;
d)umoja;
e)uwazi;
f)uwajibikaji ;na

g)lugha ya Taifa.

SOMA KWA MAKINI UTANGULIZI HUU WA RASIMU YA JAMHURI TA MUUNGANO WA TAZANIA

Kwa kuwa, sisi wananchi wa jamhuri wa muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya utu,uhuru,haki,usawa,udugu,amani,umoja na mshikamano katika Nyanja zote za maisha yetu;


Na kwa kuwa,tunaamini kuwa misingi hiyo inaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye mfumo wa kidemokrasia na utawala bora ambayo serikali yake inasimamiwa na Bunge lenye Wabunge waliochaguliwa na wanaowakilisha wananchi,na Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo kudumisha na kwamba wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu
Na kwakuwa ,tunatambua umuhimu wa kutunza mali ya mamlaka ya nchi na pamoja,kupiga vita aina zote za uharibifu,ubadhirifu na kuhimiza matumizi bora na endelevu ya rasilimali na mustakabali wa maisha ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo;
Na kwa kuwa,tunatambua umuhimu na faida za kujenga,kukuza na kuendeleza amani,umoja,urafiki na ushirikianao  miungoni mwa watanzania,mataifa mbalimbali ya Afrika na duniani kwa ujumla;
Na kwa kuwa,azma ya kujenga umoja wa bara la Afrika inadhihirishwa na Muungano wa iliyokuwa jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya watu Zanzibar;
Na  kwa kuendeleza dhamira yetu hiyo,ni muhimu:
a)kulinda,kuimarisha na kuudumisha muungano wa  nch za jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya watu wa Zanzibar;
b)kujenga Taifa huru na linalojitegemea;
c)kuimarisha na kuendeleza utawala wa sheria;
d)kukuza na kuendeleza maadili,uwajibikaji na uwazi;
e)kujenga umoja na mshikamano utakaowezesha kutimiza malengo ya kisiasa,kiuchumi ,kijamii,kimazingira na kulinda urithi kwa ujumla;
f)kujenga na kuendeleza ukuu wa mamlaka ya watu;
g)kujenga na kuendeleza utii wa mamlaka ya katiba;na
h)kuimarisha na kudumisha uzalendo kwa taifa miungoni mwa watanzania;
NA KWA KUZINGATIA,urithi tulioachiwa wa waasisi wa Taifa letu wa kujenga nchi yenye umoja wa watu wake ambao hawabaguani kwa misingi ya ukabila,dini ,rangi,jinsi au ubaguzi wa aina nyingine yoyote;
NA KUZINGATIA,uzoefu wa zaidi ya miaka hamsini ya uhuru wa Tanganyika,miaka hamsini ya mapinduzi ya Zanzibar na miaka hamsini ya muungano wa jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya watu wa Zanzibar,na uhumuhimu wa ushiriki mpana na bayana wa wananchi katika utungaji wa katiba ya jamhuri  ya muungano wa Tanzania;
HIVYO BASI,KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI WANACHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WATANZANIA kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo,na kuhakikisha kuwa jamhuri ya muungano wa Tanzania inaongozwa na serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na utawala wa sheria,kujitegemea na isiyofungamana na dini.



 TOA MAONI YAKO

Wednesday, 2 April 2014

JE?UNAWAZO GANI KATIKA HILI?UNAWAAMBIA NINI KATIKA KUTUNZA MAZINGIRA?tazama picha katika jiji la Arusha jinsi mitalo ya maji inavyokuwa kero kwa afya

Ni wazi kabisa tunatambua hili ni tatizo kubwa ingawa linachukuliwa kawaida sana,katika haki za binadamu lazima tuzingatie na mazingira yake anayoishi.



Mradi wa barabara umeletwa katika jamii ni jambo zuri sana lakini inakuwa mbaya sana kama barabara hizo zinatengenezwa bila kukamilika kabisa hii ni kuchezea fedha za umma

Hizi picha ni katika jiji la Arusha asilimia kubwa sehemu nyingi mitalo haijafunikwa kabisa jambo ambalo linasababisha kuchafua mazingira ya jiji.

weka mazingira safi ili yakuweke safi

Friday, 21 March 2014

KAULI YENU IWE TANZANIA KWANZA maneno ya DR KIKWETE KWA BUNGE MAALUMU

Baada ya kuzungumza maneno ya yakufuraisha na kujenga bungeni RAIS DR Jakay Mrisho kikwete
ni wazi kabisa alionyesha hisia jinsi anavyoipenda nchi yake baada ya kuzungumza kwa kirefu sana
 aliwaasa wabunge kuwa kauli mbiu ya kusema TANZANIA KWANZA

GARI LA ANOTHER G YAPATA AJARI UKO MKOANI NJOMBE fungua utazame picha ya ajari mbaya

 kampuni ya another G iliyopo mkoani njombe yapata pigo baada ya gari moja kupata ajari mbaya

LIVE BUNGENI RAIS DR JAKAYA MRISHO KIKWETE AKIZUNGUMZIA JUU YA SERIKARI TATU


Wednesday, 19 March 2014

DONA LA ZUA BALAA VIKOBA WALIVAMIA BUZA KWA MAMA KIBONGE,tazama picha



Ni hari isiyotegemewa na kila mtu katika mazingira yetu ,katika eneo moja lilipo BUZA maeneo ya kituo cha mama kibonge alimaarufu kama kwa dona limezua kasheshe baada ya eneo hilo kugawiwa kwa wananchi kwa ajili ya kufanya biashara ndogondogo,awali kabla maeneo haya jatolewa uongozi huo uliwatangazia watu kwa ajili ya kuandikisha majina na namba zao za simu ili waweze kuwagawia kwa utararatibu,wananchi zaidi ya 3000 waliitikia wito na kujiandikisha lakini baada ya muda kidogo utaratibu ukabadilika wakatangaza wanagawa maeneo bila kuita majina bali wanampatia mtu yeyote mwenye biashara hapo hapo jambo ili liliwakwaza baadhi ya watu walio andika majina.


Tathimini inaonyesha asilimia kubwa ya wafanya biashara hao ni wanachama mbalimbali wa VIKOBA baada ya kuwahoji asilimia kubwa ya watu walinithibitishia wao wapo katika VIKOBA .Tangu niingie vikoba sijawahi kuangaika kama jinsi nilivyokuwa katika mikopo ya saccos,benk na hata pride lakini sasa nina raha sana katika kikundi  kikoba hivyo lazima nijishughulishe ili nipate fedha ya marejesho ya hisa kila wiki,ni mama Faudhia alifunguka kwa furaha jinsi VIKOBA  inavyo mpa raha
Eneo ni kubwa linavyoonekana litahusisha michezo mbalimbali ya watoto mfano bembea,treni la umeme,na vitu vingi ambavyo wananchi walisikia kama fununu.
Mategemeo yetu eneo hili liwe kubwa kama Tandika sokoni ili nasi tuweze fanya biashara tujipatie kipato,tunamshukuru aliyejitolea kutupa maeneo kiukweli ameona mbali sana hatuna cha kumlipa ila Mungu ndo atamlipa.ni Aisha Mbeya mwanachama wa VIKOBA mkazi wa kata ya makangarawe aliongea maneno hayo kwa upole sana

Maeneo haya yanasemekana ni ya kanisa la Angrikana ,wanahabari wetu walijaribu kumtafuta kiongozi wa kanisa hakupatikana .

JE?KWA NINI SERIKALI NYINGI ZA MTAA HAZINA UBAO WA MATANGAZO KWA NJE?cheki picha katika blog

Tunapozungumzia serikali ya mtaa(local government)ni wazi kabisa wengi tunatambua tuna zungumzia serikali gani,kwa asilimia kubwa nchini serikali hii ipo kila mtaa kwa ajili ya wananchi wake na wala si kwa ajili ya viongozi wa serikalini lakini cha ajabu zaidi ni kwamba asilimia ya wananchi wengi wanaogopa kuwa karibu na serikali yao ambayo ipo kwa ajili yao wenyewe.
Mbao za matangazo aziwekwi kwa sababu ni sehemu ambayo wananchi ni rahisi kupata taarifa na kuhoji endapo taarifa sio sahii na mara nyingi taarifa zinakuwa na kasoro za kiubadhirifu.
Kuna vitu muhimu sana vya kuzingatia kama wananchi wa Tanzania hasa kwa ajili ya maendeleo yetu wenyewe kasumba kubwa ni kwamba tumenyimwa elimu ya kuelewa vitu vya msingi ili tuweze nyanyaswa pasipo na hatia,mara nyingi viongozi wa mtaa wakichaguliwa wanabadilika sana tunawanajiona tofauti na wananchi wa kawaida.
Sheria inatambua kabisa haki na wajibu wa mwananchi na viongozi,mwananchi anayo haki ya kuuliza na kuhoji swala la maendeleo katika mtaa wake pasipo kuvunja sheria ya nchi
KUMBUKA SERIKALI YA MTAA YOYOTE LAZIMA IWE NA UBAO WA MATANGAZO AMBAO UNAONYESHA MAPATO NA MATUMIZI NA TAARIFA ZINGINE MUHIMU.

Hivyo kama mwanajamii na haki yako kuuliza na kuhoji ni muhimu sana kufatilia ili kujiletea maendeleo sisi wenyewe lazima tuanze chini alafu ndo tupande juu.

Tuesday, 18 March 2014

TAKATAKA KANDO YA BARABARA UCHAFUNZI WA MAZINGIRA




Siku zote mazingira hutuzwa na watu waliozunguuka mazingira hayo,ni wazi kabisa tunatambua mazingira ukiyatunza nayo yanakutunza ila kinyume tutasema usipo ya tunza nao hayatakutunza.Yamkini tunatambua fika umuhimu wa kutunza mazingira lakini tufanyapo jambo huku tunajuwa ili nikosa maana yake tunakusudia kufanya kwa makusudi kabisa.
Kipindi cha mda mrefu sana wakaza wa buza walikuwa na kilio cha barabara ya rami yenye kurahisisha usafiri tena ikawa kama ndo sababu ya watu kutumia kama sera katika kampeni zao za kujinadi ya kwamba watatengeza barabara yenye kiwango lakini leo cha kushangaza wakazi hao wameonyesha dhahiri katika utunzaji wa mazingira ya barabara hiyo yenye kiwango cha rami.
Sehemu kubwa ya barabara watu wanatupa takataka, hili jambo ni la kushangaza sana  na nila aibu kama jamii kiujumla,mazingira ni muhimu sana kuyatunza hasa katika sehemu ambazo tunaishi kila siku, pia inakupasa kutambua mradi wowote unaotolewa na serikali kuhusiana na jamii yake inakuhusu wewe na mwengine kwa sababu kile wanachopanga serikali ni mtazamo kutoka katika jamii yake,kasumba yetu sisi watanzania ni kwamba kitu cha chochote cha serikali tunakitumia hovyo bila kujisikia uchungu kumbe tunasahau matokeo yale ni baada ya nguvu kazi zetu.

Jamani,haipendezi maneno kama haya yawe yanaludiwa kwa kila siku yatachosha watu ila tutayaludia endapo watu hawataonyesha ushirikiano lazima tuweke sheria ndogo ya kuzibiti uchafunzi wa mazingira.Mwisho kabisa napenda kuwahasa viongozi wa serikali za mitaa kutafuta maeneo maalumu ya kutupa takataka ili iwe rahisi kutunza mazingira yetu kwani kutunza mazingira ni jambo muhimu sana hasa katika kutunza afya zetu kiujumla lakini pia wananchi tuwe macho na kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzie.

Monday, 3 March 2014

KUWAFUNGA NA KUWANYANYASA SIO NJIA SAHIHI YA KUPUNGUZA USHOGA

Inawezekana ikawa ni furaha kwako kwakuwa upendi tabia ya ushoga ingawa unapenda kuzini,wengi wanasema kwamba dhambi kubwa sana kuwa shoga maana yake shoga awezi kuingia mbinguni ni wazi kabisa tofauti na mawazo ya MUNGU.Na sowezi amini kwamba mungu anaweza mchukia mtu sababu ya tabia yake.
Baadhi ya watu wamefurahishwa na kile ambacho MSEVENI amepitisha kwamba anajenga maadili kwa kwa kutaza tabia ya ushoga kwa sheria  kali,lakini tukumbuki kuwa watu wenye tabia ya ushoga ni binadam kama wewe,leo utasema vibaya kwa mashoga kwa kuwa ujui kama ndugu yako wa karibu mfano kama mtoto wako,baba yako,kaka yako mjomba wako na hata mdogo wako akawa na tabia hiyo,lakini leo unasema tuwatenge bila ya kujua ndugu zako ndo tabia yao.Binafsi si dhani kama itakuwa njia sahihi kuwanyanyasa mashoga eti kisa tabia zao,kumbuka shoga si mbaya ila tabia ya ushoga ndo ubaya wenyewe na tabia ukuwa na kusambaa,hivyo uliyefikiri kuwa kuwafunga mashoga ni sahihi basi umekosa nidhamu za haki ya binadam kwa kuwa wakosaji si mashoga tu bali hata wale wanao watumia mashoga kutimiza haja zao,KUWAFUNGA NA KUWANYANYASA SIO KUPUNGUZA MASHOGA.
kunahaja ya kuwa na SOMO LA MAADILI kwa watoto na hata vijana wa rika fulani,kuhusiana na mambo yote ambayo yanakuwa chukizo katika jamii.(MADAWA YA KULEVYA,UKIMWI,USHOGA,NA N.K)watu wajue namna yanavyopelekea mpaka kuingia katika mambo kama hayo na madhara hasa watoto wadogo ambao wanakuwa na hata vijana wanaokaribia kubarehe au wanao barehe.
kwa sababu tabia hizi chimbuko lake ni tangu utotoni.
Tuchukue hatua kabla ya tatizo kuwa kubwa.