Translate
Translate
Monday, 1 December 2014
TUJITAZAME KISHA TUTAZAME NA WENGINE
SIKU ZOTE KAZI NZURI UONGOZI MZURI, KATIKA SWALA LA UWAZI NA UWAJIBIKAJI UANZIE KWETU KWANZA NDO TWENDE KUHAMASISHA WENGINE KAMA MIONGONI MWA KAZI AMBAZO ZINA FANYWA NA TAASISI AU ASASI AU DINI FULANI ALAFU NDANI YAKE HAKUNA UKWELI NA UWAZI WA KUNYAMBULISHA MAMBO NI WAZI KABISA TUTAKUWA TUNATWANGA MAJI KWENYE KINU LAZIMA KATIKA KUFANYA KAZI NZURI YENYE MAFANIKIO LAZIMA UONGOZI NA WATU WAKE WASHIRIKIANE PAMOJA KATIKA KUPANGA MIKAKATI MAHUSUSI YA KUFIKIA LENGO KAMA KUTAKUWA NA MIZUNGUKO KATIKA KUTOA MAELEZO SAHII HILO NI TATIZO NA HATUWEZI TATUA MATATIZO MENGINE, JAMBO HILI NI LAKUZINGATIA SANA , UNAWEZA UKAWA NA MOYO WA KUJITOLEA KATIKA KAZI FULANI KWA LENGO ZURI LAKINI UNAPONYIMWA HAKI YAKO UNAKATISHWA TAMAA YA KUENDELEA NA KAZI HIVYO BASI MABADILIKO YAANZIE KWETU NDO TUPELEKE KWA WENGINE USIMAMIZI MBOVU KAZI MBOVU DAIMA.
Monday, 3 November 2014
Sunday, 2 November 2014
HALI HALISI YA MBAGALA BUS TERMINAL KATIKA WILAYA YA TEMEKE
Makala
leo asubuhi nikiwa katika safari zangu nimekerwa sana na hili la mbagala bus terminal nadhani hata wewe kama mwananchi wa mbagala unalijua hilo na linakukela pia
kwa wale ndugu zangu mliofika mbagala bus terminal mnajua hali halisi katika stand hiyo ya mabasi makubwa na madogo , ni wazi kabisa serikali inatambua kama ni wajibu wao katika uboreshaji , lakini tunasema uwajibikaji na utawala bora ni kasumba nzito sana nchi
katika kuuliza uliza kwangu inasemekana kila basi linaloingia pale linalipa ushuru kwa ajili ya stand bila shaka hata wafanyabiashara pale wanalipa ushuru wa eneo la stand yamkini hata wewe ni mmoja wapo katika sehemu fulani unalipa kodi au ushuru wa serikali , lakini kama wananchi tunahaki ya kujua fedha hizo tunazo katwa ni kwa ajili ya matumizi yapi. Mbagala inatambulika kila sehemu nje na ndani ya nchi kibiashara na hata kimapato ya nchi
kwenu wahusika wakuu katika uboreshaji wa mazingira ya mbagala bus terminal ni wazi mnapata mapato yetu lakini hamtaki kuyafanyia kazi iweje terminal kubwa kama mbagala bado inavumbi chini mpangilio mbovu wa magari hata mazingira ya usafi hakuna uduma za choo hazilidhishi?
Watanzania wenzangu bila kusimama wenyewe hatuta weza kusimamishwa sisi ndo watu wa kufanya mabadiko tuachane na mambo ya umimi tuungane kuweza kujiwekea mazingira salama wenyewe kwani uwezi mkuta mtoto wa viongozi wa kiwa katika mazingara ambayo tunayaishi sisi.
Tusisubiri kusukumwa tuanze wenyewe.
leo asubuhi nikiwa katika safari zangu nimekerwa sana na hili la mbagala bus terminal nadhani hata wewe kama mwananchi wa mbagala unalijua hilo na linakukela pia
kwa wale ndugu zangu mliofika mbagala bus terminal mnajua hali halisi katika stand hiyo ya mabasi makubwa na madogo , ni wazi kabisa serikali inatambua kama ni wajibu wao katika uboreshaji , lakini tunasema uwajibikaji na utawala bora ni kasumba nzito sana nchi
katika kuuliza uliza kwangu inasemekana kila basi linaloingia pale linalipa ushuru kwa ajili ya stand bila shaka hata wafanyabiashara pale wanalipa ushuru wa eneo la stand yamkini hata wewe ni mmoja wapo katika sehemu fulani unalipa kodi au ushuru wa serikali , lakini kama wananchi tunahaki ya kujua fedha hizo tunazo katwa ni kwa ajili ya matumizi yapi. Mbagala inatambulika kila sehemu nje na ndani ya nchi kibiashara na hata kimapato ya nchi
kwenu wahusika wakuu katika uboreshaji wa mazingira ya mbagala bus terminal ni wazi mnapata mapato yetu lakini hamtaki kuyafanyia kazi iweje terminal kubwa kama mbagala bado inavumbi chini mpangilio mbovu wa magari hata mazingira ya usafi hakuna uduma za choo hazilidhishi?
Watanzania wenzangu bila kusimama wenyewe hatuta weza kusimamishwa sisi ndo watu wa kufanya mabadiko tuachane na mambo ya umimi tuungane kuweza kujiwekea mazingira salama wenyewe kwani uwezi mkuta mtoto wa viongozi wa kiwa katika mazingara ambayo tunayaishi sisi.
Tusisubiri kusukumwa tuanze wenyewe.
Saturday, 1 November 2014
NIMELUDI SASA
Ni baada ya kupotea kidogo ili kuweka sawa mambo fulani kwa lengo la kuboresha kazi nzuri zaidi
sasa unatakiwa kuwa taayari na kufatilia blog yangu ili kuweza kupata taarifa zinazo kuhusu wewe
kama mdau wa jamii kiujumla .
Pia nachukuwa nafasi hii kuwatakaradhi watu wangu waliokuwa wanafatilia blog hii
kwa kuwanyima taarifa zinazo wahusu sasa endelea kujifunza zaidi.
ASANTE
sasa unatakiwa kuwa taayari na kufatilia blog yangu ili kuweza kupata taarifa zinazo kuhusu wewe
kama mdau wa jamii kiujumla .
Pia nachukuwa nafasi hii kuwatakaradhi watu wangu waliokuwa wanafatilia blog hii
kwa kuwanyima taarifa zinazo wahusu sasa endelea kujifunza zaidi.
ASANTE
Saturday, 26 April 2014
MKUKUTA NI NINI?soma ujilidhishe
MKUKUTA ni nini?NI kifupisho cha maneno ya Kiswahili yenye maana ya
mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini Tanzania.
MKUKUTA awamu ya 1(2005/06-2009/10)ulilenga katika kukuza uchumi
,kupunguza umasikini wa kipato ,ubora wa maisha ya watu na ustawi wa jamii
pamoja na kuimarisha utawala bora na uwajibikaji .utekelezaji wake ulienda
sambamba na uandaaji wa ripoti za kila mwaka zikiainisha uzoefu ,mafanikio na
changamoto.
Kila mwaka ripoti zilijadiliwa na wadau mbalimbali katika makongamano na
mikutano ya kitaifa ya sera.Maoni kutoka kwenye mapitio na mijadala hiyo
yalitumika katika kuboresha mpango wa mwaka uliofuata.
MKUKUTA inachangia katika utekelezaji wa dira ya taifa ya
maendeleo(2025)na malengo ya maendeleo ya millennia (2015).
Tuesday, 15 April 2014
SOMA UJUE VYANZO VYA HAKI VYA MWANANCHI WA TANZANIA
HAKI ZA UHALALI WA MWANANCHI KUFATILIA MATUMIZI YA RASILIMALI ZA
UMMA(PETS)
Haki ni stahili ya binadam .Hii inamaanisha kuwa mtu ana haki kwa kuwa
anastahili ya kutenda jambo Fulani,au wengine wanatakiwa kutenda au kumtendea
jambo Fulani katika hali Fulani . Haki zinaweza kuwa binafsi au za jumla . Kwa
lugha rahisi ,tunasema kuwa haki ni stahili za msingi ambazo binadamu yeyote Yule
bila kujali jinsia ,umri ,itikadi,dini,rangi ,kabila au aina yoyote ya utofauti
huzaliwa nazo na hazitolewi na mtu na wala haziwezi kuondolewa na mtu kwa
sababu yeyote .vivyo hivyo ,uhalali wa mtu kufanyanya au kufanyiwa jambo Fulani
,unatikana na stahili ambayo mtu au wattu wanakuwa nayo kw mujibu wa sheria
,sera kanuni ,taratibu au muongozo husika,Ni kwa muktadha huo,wananchi kupitia
sheria ,sera,matamko ,mikataba ,kanunui na miongozo mbalimbali ,wanapata haki
na uhalali wa kufuatilia matumizi ya rasilimali za umma kila mara wanapoona
inafaa kufanya hivyo
NB;VYANZO VYA
HAKI
a)mila na desturi
b)katiba ya nchi
c)sera na miongozo
c)sheria za nchi
d)kanuni na mikataba ya kitaifa /kimataifa
Saturday, 12 April 2014
MIFUMO YA TATHIMINI NA UFATILIAJI WA RASILIMALI ZA UMMA(PETS)
Kuna aina kadhaa za mifumo ya tathmini ambayo inatumiwa kulingana na
mahitaji au mazingira ya sehemu husika.mifumo hiyo ni kama vile;ufatiliaji wa
Matumizi ya fedha za umma(public expenditure system and survey),ushirikishwaji
wa jamii ya vijiji katika tathmini(participatory rural appraisal(PRA),tathmini
ya uwajibikaji wa jamii(social accountability monitoring)na PIMA KADI
Mifumo yote hiyo imeainishwa utaratibu ambao unaweza kutumika katika
kukusanya taarifa inayokusudiwa katika kuijenga jamii uwezo,kuiwezesha kuwa na
kauli na kushiriki ipasavyo katika kutathimini na kuiwajibisha mamlaka husika
pale inapobainika kuwa rasilimali za umma zimetumika kinyume na jinsi ilivyokusudiwa.Mifumo yote
hiyo ni sahihi na inafaa kutumika kilingana na chaguo la sehemu husika.
Katika muongozo huu ,mfumo mkuu wa tathmini utakaotumika na
tutakaojikita nao zaidi ni mfumo wa ufatiliaji wa matumizi ya fedha za umma au
PETS,pia tutaangalia kwa undani kuhusu zana ya PIMA KADI na jinsi inavyotumika
kama nyenzo ya kukusanya taarifa.
Kwa ujumla PETS na mifumo yake imesaidia kujibu maswali ambayo mara
nyingi wananchi wamekuwa wanajiuliza ili kupima tathimini ya fedha zilizopangwa
au kutumika na matokeo husika .Hivyo kupitia PETS wananchi wanaweza kufanya
tathimini na kupata ufumbuzi wa maswali yanayowakabili kuhusu mgawanyo wa
matumizi ya rasilimali zao. Baadhi ya maswali ambayo wananchi hujiuliza ni kama
yafuatayo
1)je,fedha na rasilimali za umma huwafikia wananchi hususani wale wa
ngazi ya chini mfano wanawake na watoto kama ilivyokusudiwa ?
2)je,rasilimali fedha na rasilimali zingine zinawafikia wananchi kwenye
maeneo husika kwa mtizamo wa kijinsia?
Utaona kuwa swali la kwanza linalohoji mtiririko wa fedha na rasilimali
za umma zitolewazo ama na serikali kuu au wafadhili au wabia wa kimaendeleo ili
kugharamia miradi ya maendeleo katika kijiji,kata.Mantiki yake ni kutaka
kufahamu ni kiasi gani cha fedha na rasilimali za umma zimewafikia walengwa au
watoa huduma,kama vile hospitali,shule ,maji ,barabara nk kama ilivyokusudiwa.
Katika kufanya tathmini na kujiuliza maswali hayo ,na iwapo kuhoji huko
kunaweza kukasababisha uchunguzi na ikadhihirika kuwepo na utofauti ya fedha
zilizotolewa katika ngazi ya serikali kuu na kiasi kilichopelekwa kwa watoa
huduma katika ngazi za nchini,huo unaitwa uvujaji.Hii inamaanisha kuwa baadhi
ya pesa au rasilimali zilizotolewa kwa ajili ya miradi ya
maendeleo,hazijatumika kulingana na sera au maleng yaliyokusudiwa na serikali
au mamlaka husika.maana yake ni kuwa fedha au rasilimali hizi zimekwapuliwa
katika ngazi Fulani ya kiutawala,inaweza kuwa wilayani au mikoani.
Hali kadhalika ,swali la pili linalenga zaidi katika uchambuzi.Lengo ni
kubainisha kwa nini uvujaji hujitokeza.Mara nyingi,hujibu maswali kama vile
,kwa nini uvujaji hutokea katika baadhi ya halmashauri zaidi ya zingine?Au kwa
nini shule ,halmashauri kadhaa hupokea fedha na rasilimali nyingi kuliko
zingine
Kwa kufanya utambuzi huo ,mfumo unawezesha namna ya kufatilia ili
kupunguza uvujaji na kuboresha utendaji na uwajibikaji katika ngazi ya
ki-serikali /uongozi /utawala husika
Hivyo basi,ili kuondosha mianya ya rushwa na kuimarisha utawala bora
katika ngazi zote husika za uongozi,ni vyema kutambua mianya ya rushwa,ambapo
suala la kuwajengea uwezo wananchi au wapokeaji wa huduma,litaweza kusaidia
usimamizi na udhibiti wa rasilimali katika maeneo yote.Pia kwa kutumia mfumo wa
PETs wananchi watadai taarifa za matumizi kulingana na huduma zitolewazo ,pia
watahoji kiwango cha utendaji kazi wanapokuwa na shaka ,hivyo kuzuia kushamiri
kwa rushwa kwa viongozi wao.
Wednesday, 9 April 2014
UTAWALA WA KIDEMOKRASIA KATIKA JAMII NINI?soma ufahamu.
Mwananchi ana wajibu na majukumu yake kuhakikisha kuwa kiongozi
aliyemchagua au kuteuliwa anatimiza wajibu wake ipasavyo katika viwango
vinavyokubalika katika eneo la kijiji/mtaa.Kila mwananchi ana wajibu wa kupanga
na kukataa kila aina ya uovu katika jamii ikiwemo rushwa,uonevu,wizi,ubadhilifu
wa mali za umma nay a watu binafsi.
Mwananchi pia wana jukumu la kudai na kupigania haki zao za wananchi
wengine kutoa malalamiko na kuuliza maswalijuu ya mambo mbalimbali vya jamii na
kiserikali.Wananchi wanashiriki katika serikali za mitaa kupitia vikao au
mikutano mbalimbali ambapo hujadili na kutoa mapendekezo yao kuhusu mipango na
matatizo yanayowakabili kwa namna moja au nyingine ili kuweza kupatiwa ufumbuzi
na kurahisiha uboreshaji wa huduma za kijamii katika maeneo yao wanamoishi.
VIZURI SOMO LA DEMOKRASIA TUNGEIPIGANIA MPAKA VIONGOZI WAIFATE IPASVYO
Monday, 7 April 2014
SAFISHA JIJI TANDIKA SOKONI WAKIMBIZANA NA MIZIGO tazama picha
Operesheni ya safisha jiji katika mji wa dar es salaam umekuwa gumzo kubwa sana katika maeneo mbalimbali jijini dar es salaam baada ya wafanyabiashara kukimbizana na mizigo yao ili kuepusha shari ya serikali,
katika eneo la Tandika sokoni jana asubuhi wafanyabiashara hao ambao waliweka biashara zao katika maeneo yasiyo sahihi walikumbwa na operesheni hiyo ya kusafisha jiji,pia katika maeneo ya mbagala safisha jiji ilifanyika kupitia jeshi la polisi likisaidiaana na jeshi la wagambo.
Friday, 4 April 2014
JE? NI KWELI JAMHURI YA MUUNGANO INAENZI NA KUZINGATIA TUNU HIZI soma uzijue tunu za Taifa
JAMHURI YA MUUNGANO ITAENZI NA KUZINGATIA TUNU ZA TAIFA ZIFUATAVYO:
a)utu;
b)azalendo;
c)uadilifu;
d)umoja;
e)uwazi;
f)uwajibikaji ;na
g)lugha ya Taifa.
SOMA KWA MAKINI UTANGULIZI HUU WA RASIMU YA JAMHURI TA MUUNGANO WA TAZANIA
Kwa kuwa,
sisi wananchi wa jamhuri wa muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati
kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya
utu,uhuru,haki,usawa,udugu,amani,umoja na mshikamano katika Nyanja zote za
maisha yetu;
Na
kwa kuwa,tunaamini kuwa misingi hiyo inaweza tu kutekelezwa
katika jamii yenye mfumo wa kidemokrasia na utawala bora ambayo serikali yake
inasimamiwa na Bunge lenye Wabunge waliochaguliwa na wanaowakilisha wananchi,na
Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo
kudumisha na kwamba wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu
Na kwakuwa ,tunatambua
umuhimu wa kutunza mali ya mamlaka ya nchi na pamoja,kupiga vita aina zote za
uharibifu,ubadhirifu na kuhimiza matumizi bora na endelevu ya rasilimali na
mustakabali wa maisha ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo;
Na
kwa kuwa,tunatambua umuhimu na faida za kujenga,kukuza na
kuendeleza amani,umoja,urafiki na ushirikianao
miungoni mwa watanzania,mataifa mbalimbali ya Afrika na duniani kwa
ujumla;
Na kwa
kuwa,azma ya kujenga umoja wa bara la Afrika
inadhihirishwa na Muungano wa iliyokuwa jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya
watu Zanzibar;
Na kwa kuendeleza dhamira yetu hiyo,ni muhimu:
a)kulinda,kuimarisha na kuudumisha muungano wa nch za jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya
watu wa Zanzibar;
b)kujenga Taifa huru na linalojitegemea;
c)kuimarisha na kuendeleza utawala wa sheria;
d)kukuza na kuendeleza maadili,uwajibikaji na uwazi;
e)kujenga umoja na mshikamano utakaowezesha kutimiza
malengo ya kisiasa,kiuchumi ,kijamii,kimazingira na kulinda urithi kwa ujumla;
f)kujenga na kuendeleza ukuu wa mamlaka ya watu;
g)kujenga na kuendeleza utii wa mamlaka ya katiba;na
h)kuimarisha na kudumisha uzalendo kwa taifa miungoni
mwa watanzania;
NA
KWA KUZINGATIA,urithi tulioachiwa wa waasisi wa Taifa letu wa
kujenga nchi yenye umoja wa watu wake ambao hawabaguani kwa misingi ya
ukabila,dini ,rangi,jinsi au ubaguzi wa aina nyingine yoyote;
NA
KUZINGATIA,uzoefu wa zaidi ya miaka hamsini ya uhuru wa
Tanganyika,miaka hamsini ya mapinduzi ya Zanzibar na miaka hamsini ya muungano
wa jamhuri ya Tanganyika na jamhuri ya watu wa Zanzibar,na uhumuhimu wa
ushiriki mpana na bayana wa wananchi katika utungaji wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania;
HIVYO
BASI,KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE
MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI WANACHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WATANZANIA
kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni
ya kujenga jamii kama hiyo,na kuhakikisha kuwa jamhuri ya muungano wa Tanzania
inaongozwa na serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na utawala wa
sheria,kujitegemea na isiyofungamana na dini.
TOA MAONI YAKO
Wednesday, 2 April 2014
JE?UNAWAZO GANI KATIKA HILI?UNAWAAMBIA NINI KATIKA KUTUNZA MAZINGIRA?tazama picha katika jiji la Arusha jinsi mitalo ya maji inavyokuwa kero kwa afya
Ni wazi kabisa tunatambua hili ni tatizo kubwa ingawa linachukuliwa
kawaida sana,katika haki za binadamu lazima tuzingatie na mazingira yake
anayoishi.
Mradi wa barabara umeletwa katika jamii ni jambo zuri sana lakini
inakuwa mbaya sana kama barabara hizo zinatengenezwa bila kukamilika kabisa hii
ni kuchezea fedha za umma
Friday, 21 March 2014
KAULI YENU IWE TANZANIA KWANZA maneno ya DR KIKWETE KWA BUNGE MAALUMU
Baada ya kuzungumza maneno ya yakufuraisha na kujenga bungeni RAIS DR Jakay Mrisho kikwete
ni wazi kabisa alionyesha hisia jinsi anavyoipenda nchi yake baada ya kuzungumza kwa kirefu sana
aliwaasa wabunge kuwa kauli mbiu ya kusema TANZANIA KWANZA
ni wazi kabisa alionyesha hisia jinsi anavyoipenda nchi yake baada ya kuzungumza kwa kirefu sana

Wednesday, 19 March 2014
DONA LA ZUA BALAA VIKOBA WALIVAMIA BUZA KWA MAMA KIBONGE,tazama picha
Ni hari isiyotegemewa na kila mtu katika mazingira yetu ,katika eneo moja lilipo BUZA maeneo ya kituo cha mama kibonge alimaarufu kama kwa dona limezua kasheshe baada ya eneo hilo kugawiwa kwa wananchi kwa ajili ya kufanya biashara ndogondogo,awali kabla maeneo haya jatolewa uongozi huo uliwatangazia watu kwa ajili ya kuandikisha majina na namba zao za simu ili waweze kuwagawia kwa utararatibu,wananchi zaidi ya 3000 waliitikia wito na kujiandikisha lakini baada ya muda kidogo utaratibu ukabadilika wakatangaza wanagawa maeneo bila kuita majina bali wanampatia mtu yeyote mwenye biashara hapo hapo jambo ili liliwakwaza baadhi ya watu walio andika majina.
Tathimini inaonyesha asilimia kubwa ya wafanya biashara hao ni wanachama
mbalimbali wa VIKOBA baada ya kuwahoji asilimia kubwa ya watu walinithibitishia
wao wapo katika VIKOBA .Tangu niingie
vikoba sijawahi kuangaika kama jinsi nilivyokuwa katika mikopo ya saccos,benk
na hata pride lakini sasa nina raha sana katika kikundi kikoba hivyo lazima nijishughulishe ili nipate
fedha ya marejesho ya hisa kila wiki,ni mama Faudhia alifunguka kwa furaha
jinsi VIKOBA inavyo mpa raha
Eneo ni kubwa linavyoonekana litahusisha michezo mbalimbali ya watoto
mfano bembea,treni la umeme,na vitu vingi ambavyo wananchi walisikia kama
fununu.
Mategemeo
yetu eneo hili liwe kubwa kama Tandika sokoni ili nasi tuweze fanya biashara
tujipatie kipato,tunamshukuru aliyejitolea kutupa maeneo kiukweli ameona mbali
sana hatuna cha kumlipa ila Mungu ndo atamlipa.ni Aisha
Mbeya mwanachama wa VIKOBA mkazi wa kata ya makangarawe aliongea maneno hayo
kwa upole sana
Maeneo haya yanasemekana ni ya kanisa la Angrikana ,wanahabari wetu
walijaribu kumtafuta kiongozi wa kanisa hakupatikana .
JE?KWA NINI SERIKALI NYINGI ZA MTAA HAZINA UBAO WA MATANGAZO KWA NJE?cheki picha katika blog
Tunapozungumzia serikali ya mtaa(local government)ni wazi kabisa wengi
tunatambua tuna zungumzia serikali gani,kwa asilimia kubwa nchini serikali hii
ipo kila mtaa kwa ajili ya wananchi wake na wala si kwa ajili ya viongozi wa
serikalini lakini cha ajabu zaidi ni kwamba asilimia ya wananchi wengi
wanaogopa kuwa karibu na serikali yao ambayo ipo kwa ajili yao wenyewe.
Mbao za matangazo aziwekwi kwa sababu ni sehemu ambayo wananchi ni
rahisi kupata taarifa na kuhoji endapo taarifa sio sahii na mara nyingi taarifa
zinakuwa na kasoro za kiubadhirifu.
Kuna vitu muhimu sana vya kuzingatia kama wananchi wa Tanzania hasa kwa
ajili ya maendeleo yetu wenyewe kasumba kubwa ni kwamba tumenyimwa elimu ya
kuelewa vitu vya msingi ili tuweze nyanyaswa pasipo na hatia,mara nyingi
viongozi wa mtaa wakichaguliwa wanabadilika sana tunawanajiona tofauti na
wananchi wa kawaida.
Sheria inatambua kabisa haki na wajibu wa mwananchi na
viongozi,mwananchi anayo haki ya kuuliza na kuhoji swala la maendeleo katika
mtaa wake pasipo kuvunja sheria ya nchi
KUMBUKA SERIKALI YA MTAA YOYOTE LAZIMA IWE NA UBAO WA MATANGAZO AMBAO
UNAONYESHA MAPATO NA MATUMIZI NA TAARIFA ZINGINE MUHIMU.
Hivyo kama mwanajamii na haki yako kuuliza na kuhoji ni muhimu sana
kufatilia ili kujiletea maendeleo sisi wenyewe lazima tuanze chini alafu ndo
tupande juu.
Tuesday, 18 March 2014
TAKATAKA KANDO YA BARABARA UCHAFUNZI WA MAZINGIRA
Siku zote mazingira hutuzwa na watu
waliozunguuka mazingira hayo,ni wazi kabisa tunatambua mazingira ukiyatunza
nayo yanakutunza ila kinyume tutasema usipo ya tunza nao hayatakutunza.Yamkini
tunatambua fika umuhimu wa kutunza mazingira lakini tufanyapo jambo huku
tunajuwa ili nikosa maana yake tunakusudia kufanya kwa makusudi kabisa.
Kipindi cha mda mrefu sana wakaza wa buza walikuwa na kilio cha barabara ya rami yenye kurahisisha usafiri tena
ikawa kama ndo sababu ya watu kutumia kama sera katika kampeni zao za kujinadi
ya kwamba watatengeza barabara yenye kiwango lakini leo cha kushangaza wakazi hao wameonyesha dhahiri katika utunzaji wa mazingira ya barabara hiyo yenye kiwango cha rami.
Sehemu kubwa ya barabara watu
wanatupa takataka, hili jambo ni la kushangaza sana na nila aibu kama jamii kiujumla,mazingira ni
muhimu sana kuyatunza hasa katika sehemu ambazo tunaishi kila siku, pia
inakupasa kutambua mradi wowote unaotolewa na serikali kuhusiana na jamii yake
inakuhusu wewe na mwengine kwa sababu kile wanachopanga serikali ni mtazamo
kutoka katika jamii yake,kasumba yetu sisi watanzania ni kwamba kitu cha
chochote cha serikali tunakitumia hovyo bila kujisikia uchungu kumbe tunasahau
matokeo yale ni baada ya nguvu kazi zetu.
Jamani,haipendezi maneno kama haya
yawe yanaludiwa kwa kila siku yatachosha watu ila tutayaludia endapo watu
hawataonyesha ushirikiano lazima tuweke sheria ndogo ya kuzibiti uchafunzi wa
mazingira.Mwisho kabisa napenda kuwahasa viongozi wa serikali za mitaa kutafuta
maeneo maalumu ya kutupa takataka ili iwe rahisi kutunza mazingira yetu kwani
kutunza mazingira ni jambo muhimu sana hasa katika kutunza afya zetu kiujumla
lakini pia wananchi tuwe macho na kila mmoja awe mlinzi kwa mwenzie.
Monday, 3 March 2014
KUWAFUNGA NA KUWANYANYASA SIO NJIA SAHIHI YA KUPUNGUZA USHOGA
Inawezekana ikawa ni furaha kwako kwakuwa upendi tabia ya ushoga ingawa unapenda kuzini,wengi wanasema kwamba dhambi kubwa sana kuwa shoga maana yake shoga awezi kuingia mbinguni ni wazi kabisa tofauti na mawazo ya MUNGU.Na sowezi amini kwamba mungu anaweza mchukia mtu sababu ya tabia yake.
Baadhi ya watu wamefurahishwa na kile ambacho MSEVENI amepitisha kwamba anajenga maadili kwa kwa kutaza tabia ya ushoga kwa sheria kali,lakini tukumbuki kuwa watu wenye tabia ya ushoga ni binadam kama wewe,leo utasema vibaya kwa mashoga kwa kuwa ujui kama ndugu yako wa karibu mfano kama mtoto wako,baba yako,kaka yako mjomba wako na hata mdogo wako akawa na tabia hiyo,lakini leo unasema tuwatenge bila ya kujua ndugu zako ndo tabia yao.Binafsi si dhani kama itakuwa njia sahihi kuwanyanyasa mashoga eti kisa tabia zao,kumbuka shoga si mbaya ila tabia ya ushoga ndo ubaya wenyewe na tabia ukuwa na kusambaa,hivyo uliyefikiri kuwa kuwafunga mashoga ni sahihi basi umekosa nidhamu za haki ya binadam kwa kuwa wakosaji si mashoga tu bali hata wale wanao watumia mashoga kutimiza haja zao,KUWAFUNGA NA KUWANYANYASA SIO KUPUNGUZA MASHOGA.
kunahaja ya kuwa na SOMO LA MAADILI kwa watoto na hata vijana wa rika fulani,kuhusiana na mambo yote ambayo yanakuwa chukizo katika jamii.(MADAWA YA KULEVYA,UKIMWI,USHOGA,NA N.K)watu wajue namna yanavyopelekea mpaka kuingia katika mambo kama hayo na madhara hasa watoto wadogo ambao wanakuwa na hata vijana wanaokaribia kubarehe au wanao barehe.
kwa sababu tabia hizi chimbuko lake ni tangu utotoni.
Tuchukue hatua kabla ya tatizo kuwa kubwa.
Baadhi ya watu wamefurahishwa na kile ambacho MSEVENI amepitisha kwamba anajenga maadili kwa kwa kutaza tabia ya ushoga kwa sheria kali,lakini tukumbuki kuwa watu wenye tabia ya ushoga ni binadam kama wewe,leo utasema vibaya kwa mashoga kwa kuwa ujui kama ndugu yako wa karibu mfano kama mtoto wako,baba yako,kaka yako mjomba wako na hata mdogo wako akawa na tabia hiyo,lakini leo unasema tuwatenge bila ya kujua ndugu zako ndo tabia yao.Binafsi si dhani kama itakuwa njia sahihi kuwanyanyasa mashoga eti kisa tabia zao,kumbuka shoga si mbaya ila tabia ya ushoga ndo ubaya wenyewe na tabia ukuwa na kusambaa,hivyo uliyefikiri kuwa kuwafunga mashoga ni sahihi basi umekosa nidhamu za haki ya binadam kwa kuwa wakosaji si mashoga tu bali hata wale wanao watumia mashoga kutimiza haja zao,KUWAFUNGA NA KUWANYANYASA SIO KUPUNGUZA MASHOGA.
kunahaja ya kuwa na SOMO LA MAADILI kwa watoto na hata vijana wa rika fulani,kuhusiana na mambo yote ambayo yanakuwa chukizo katika jamii.(MADAWA YA KULEVYA,UKIMWI,USHOGA,NA N.K)watu wajue namna yanavyopelekea mpaka kuingia katika mambo kama hayo na madhara hasa watoto wadogo ambao wanakuwa na hata vijana wanaokaribia kubarehe au wanao barehe.
kwa sababu tabia hizi chimbuko lake ni tangu utotoni.
Tuchukue hatua kabla ya tatizo kuwa kubwa.
Subscribe to:
Posts (Atom)