Translate
Translate
Saturday, 18 April 2015
BARABARA ZA JAZWA VIFUSI VYA MATOPE MTAA WA MAKANGARAWE WILAYA YA TEMEKE
Juhudi za maendeleo mtaa wa Makangarawe Wilaya ya Temeke Jijini Dar es salaam Serikali imejaza vifusi barabara za mtaa wa Makangarawe jinsi ambavyo wananchi wa maeneo hayo wakilalamika kuwa vifusi hivyo ni matope matupu kipindi cha mvua zikianza kunyesha.
Juhudi hizo za serikali ziliongozwa na mwenyekiti wa mtaa kuhakikisha zoezi ilo linakamilika.
Hitambulike kuwa fedha zinazotumika katika ujenzi huu ni fedha za wananchi hivyo kuweka vifusi ambavyo vinaongeza gharama ni ufujaji wa fedha za umma pasipo malengo, Ni wazi kabisa uwekaji huu wa vifusi ni wakibabaishaji ambao matokeo yake ni matumizi mabaya ya fedha.
Wananchi wanahaki wa kukemea jambo kama ili na kuligomea ili kuonesha msimamo wao ili mambo kama haya ya matumizi mabaya ya fedha yasijitokeze kama serikali inaamuwa kuweka vifusi barabara za mtaa basi hihakikishe inaweka kifusi cha uhakika na cha kudumu chenye mwendelezo kuliko kuweka matope ambayo na chafuzi katika mazingira yetu
Wananchi inawapasa watambue MATUMIZI MABAYA NI UBADHILIFU hivyo vipigwe vita tabia hii.
WANAFUNZI HATARINI NA MAGONJWA YA MRIPUKO SHULENI
Ni katika hari ya kutisha sana ambayo mwandishi amethibitisha hatari iyo ambayo inapelekea magonjwa ya mripuko kama kipindupindu hata magonjwa ambayo yataendana na mazingira machafu pasipo kutuzwa . Hari hii imejionesha katika baadhi ya shule za wilaya ya Temeke jijini Dar es salaam jambo ambalo ni hatari sana kwa afya za watoto ambao wapo shuleni .
inabidi kushirikiana ili kuweza kuhakikisha mazingira salama na yenye kuleta afya bora sehemu zote zinazohitaji huangalizi ili kuhepusha baraa la magonjwa ya mripuko mashuleni
ASANTE
Friday, 13 February 2015
MRADI WA MAJI SAFI MAKANGARAWE NI TATIZO KWA WANANCHI
Tatizo la
Maji safi Mtaa wa Makangarawe, katika Kata ya Makangarawe Wilaya ya Temeke jiji
Dar es salaam umezidi kuwa ni shida kwa wananchi, jambo ambalo linapelekea
wananchi wengi kutumia visima vya watu binafsi ambavyo usalama wa maji si mzuri
kiafya .
Akizungumza
kwenye mkutano wa wananchi mwenyekiti wa sasa Ndugu Juma Mohamed Kibanda juu ya
tatizo la mradi huo kufika huko alisema”hii inatokana na usimamizi mbovu wa
uongozi uliopita madarakani ,uongozi kukosa uwazi na uwajibikaji jambo ambalo
limepelekea mradi huu wa maji safi na salama kufa na wananchi wetu kuangaika”
Baadhi ya
mfumo wa mabomba ya maji yamepasuka kusabisha maji mengi kuvuja na kusambaa
maeneo mbalimbali ya mtaa, na kusababisha uchafuzi wa mazingira katika maeneo
hayo ambapo ni hatari kwa afya ya jamii iliyo zunguka maeneo hayo.
Uongozi
utambue wananchi wako katika mazingira hatarishi ya kiafya na hata upatikanaji
wa maji safi na salama hivyo iwe ni changamoto kwao ili kutafuta ufumbuzi wa
tija kuondoa tabu hiyo.
Na; Joseph
malisa
Wednesday, 11 February 2015
TASAF MTAA WA MAKANGARAWE TEMEKE WAZUA MASWALI MENGI
TASAF MTAA WA MAKANGARAWE TEMEKE
WAZUA MASWALI MENGI
Mpango wa
serikali wa kunusuru kaya maskini awamu ya tatu (TASAF) ukiwa katika
utekelezaji wake wa kuhakikisha wanawafikia walengwa wa mradi huo ambao kaya
maskini umepelekea kuwemo kwa maswali mengi ya msingi kutoka kwa baadhi
ya wananchi walio hudhuria kikao hicho mtaa Makangarawe,Kata ya Makangarawe, Wilaya Temeke Dar es salaam.
Akizungumza katika mkutano mwenyekiti wa mtaa Juma Mohamed Kibanda alisema"Mpango huu wa TASAF ni mpango wa kunusuru kaya maskini ambao kwa sasa umetufika wanamakangarawe hivyo tushirikiane katika kufikia lengo na kuwafikia walengwa"aliendelea kusema "Mpango huu ni wamendeleo hasa katika kaya maskini ". Akizungumza mwezeshaji wa TASAF ambae alielezea malengo
na faida za mpango huo wa TASAF. Jambo ambalo lilizua maswali
mengi na hoja za msingi kutoka kwa wanajamii wa Makangarawe ili
kujilidhisha kama mpango huo ni waukweli au ni jambo la kisiasa ambalo linaleta
mkanganyiko kutokana na ukaribu wa uchaguzi jambo ambalo lishawahi kujitokeza
mwaka 2005 .
Wednesday, 7 January 2015
MAMBO KUMI NA MOJA YA KUZINGATIA KABLA YA KUFANYA PETS (VIEW BLOG)
UTARATIBU WA
WANANCHI KUENDESHA PETS
MASUALA YA
KUZINGATIA KABLA YA KUFANYA PETS
· Unda kamati au kikundi cha PETS
inayojumuisha uwakilishi wa makundi yote wakiwemo wanawake na vijana.
· Ainisha/bainisha sekta husika kwa
ajili ya ufatiliaji
· Bainisha namna ya kufuatilia na
kupata taarifa za kutosha kuhusu hali halisi ya sehemu husika kabla ua
ufatiliaji
· Zingatia jinsi/namna ya kufanya
ufuatiliaji
· Tambua wapi pa kwenda kwa ajili ya
kupata taarifa husika
· Nini / kitu gani cha kuuliza
· Nini kifanyike kuhamasisha umma
· Jinsi ya kutoa mrejesho na kusambaza
taarifa
· Hatua za kuchukua (ushawishi na
utetezi)
· Kitu gani au nini kimebadilika?
· Vyanzo mbalimbali vya taarifa
(TAKUKURU, TAMISEMI nk)
Tuesday, 6 January 2015
MALENGO YA UFUATILIAJI- PETS
PETS imethibitika kuwa ni kati ya zana na
nyenzo muhimu katika ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali za umma , hasa pale
inapofanyika kwa mitizamo wa kijinsia . Hivyo basi , PETS inalenga kufanikisha
yafuatayo;
Ø Kuboresha utoaji huduma ; kufuatilia matumizi ya fedha au rasilimali za umma kwa
mtizamo wa kijinsia , kunasaidia sana kuchochea uboreshaji wa utoaji wa huduma
mbalimbali za kijamii kwa ubora uliokusudiwa . vile vile kuhakikisha kuwa
rasilimali zimeenda kutekeleza lengo kusudiwa na kuhakiki thamani halisi ya
fedha zilizotumika.
Ø Kuhakiki utendaji wa serikali na mamlaka husika; mfumo huu unasaidia sana katika
kuhakiki utendaji wa serikali na mamlaka husika ,hasa katika ngazi za vitongoji
na vijiji au katika vikundi vidogo vidogo , kwa kusoma nyaraka , ripoti na
taarifa mbalimbali za utekelezaji.
Ø Kukuza uwajibikaji; Hii inaanzia kwa wananchi kwa
maana ya wanawake , wanaume , vijana , walemavu na makundi mengine yaliyoko
pembezoni , ambapo hushiriki moja kwa moja katika kuhoji serikali .sanjali na
hilo huhakikisha kwamba viongozi wanatenda kila ambacho wanapaswa kutenda
kulingana na mipango.
Ø Kuwezesha uandaaji wa mipango shirikishi ya maendeleo; Taarifa zinawafanya wananchi waweze kushiriki
vizuri katika uandaaji wa mipango ,au katika kubaini aina ya miradi
itakayotekelezwa kwenye jamii hisika
Friday, 2 January 2015
JE? TANZANIA INA UTAWALA BORA click usome kujua nini utawala bora
UTAWALA BORA
Utawala bora ni matumizi ya uwezo
(mamlaka)wa kiserikali katika jitihada za kuongeza na kutumia rasilimali hizo
ili kuboresha maisha ya wananchi
MISINGI YA
UTAWALA BORA
v Utawala wa kidemokrasia
v Ushirikishwaji wa umma
v Utawala wa kisheria
v Haki na usawa kwa watu wote
v Uwazi katika kuendesha shughuli za
maendeleo
v Uwajibikaji katika utendaji
v Uadilifu
Misingi hii ikizingatiwa
na kufanyiwa utekelezaji lazima mabadiliko yataonekana
Ili utawala bora uwe na sifa za kupendeza na kuendwa na wananchi lazima uzingatie Misingi ya utawala bora.
SOMA UFAHAMU KWA KINA JUU YA KAMATI ZA SERIKALI ZINAVYOKWENDA KINYUME NA SHERIA ZA NCHI kwa faida yetu sote
KAMATI ZA HALMASHAURI YA KIJIJI/KAMATI YA MTAA
Ø Kuna kamati tatu za halmashauri ya
kijiji/mtaa kisheria
Ø Kamati ya fedha,mipango na uchumi
,huduma za jamii na shughuli za kujitegemea na ulinzi na usalama
Ø Mkutano mkuu wa kijiji/mkutano wa
wakazi wa mtaa una uwezo wa kuagiza halmashauri ya kijij/kamati ya mtaa kuundaa
kamati ya muda kwa shughuli maalum au halmashauri yenyewe inaweza kuunda kukiwa
na haja ya kufanya hivyo.
Ø Idadi ya wajumbe katika kamati
inashauriwa wasipungue wajumbe watatu 3 na wasizidi wajumbe watano 5
Ø Kamati za kisheria inafaa ziongozwe
na mjumbe wa halmashauri ya kijiji /kamati y mtaa
Ø Inashauriwa wenyekiti wa kijiji /mtaa
, wenyeviti wa vitongoji wasiwe
wenyeviti wa kamati mbalimbali ili kutolimbikiza madaraka yote kwa halmashauri
ya kijiji/kamati ya mtaa
Ø Wananchi wakaida wanaweza kuwa wajumbe wa kamati au
wanaweza kuitwa kutoa ushauri kwenye vikao vya kamati
Ø
Kamati
zinaweza kukutana mara kwa mara kutunza kumbukumbu na kuendesha vikao kwa
kushauriwa na afisa mtendaji wa kijiji (VEO)/ Afisa mtendaji wa mtaa(MEO)
Thursday, 1 January 2015
JE? WAJUA WAJIBU WETU KWENYE SERIKALI ZA MTAA/KIJIJI? soma kwa utulivu utagundua mapungufu yetu na ya serikali usika
Mwananchi ana
wajibu na majukumu yake kuhakikisha kuwa kiongozi aliyemchagua au kuteuliwa
anatimiza wajibu wake ipasavyo katika viwango vinavyokubalika katika eneo la
kijiji/mtaa kulingana na mipango na makibaliano ya vikao vya kisheria ya kijij
na mtaa.
Kila mwananchi
ana wajibu wa kupinga na kukataa kila aina ya uovu kayika jamii ikiwemo
rushwa,uonevu wizi ubadhilifu wa mali za umma nay a watu binafsi.
Wananchi pia
wana jukumu la kudai na kupigania haki zao na za wananchi wengine kutoa
malalamiko na kuuliza maswali juu ya mambo mbalimbali yananoendelea kijijini au
kwenye mtaa kupitia vyombo mbalimbali vya kijamii na kiserikali. Wananchi wanashiriki
katika serikali za mitaaa kupitia vikao au mikutano mbalimbali ambapo hujadili
na kutoa mapendekezo yao kuhusu mipango
na matatizo yanayowakabili kwa mamna moja au nyingine ili kuweza kupatiwa
ufumbuzi na kurahisisha uboreshaji wa huduma za kijamii katika maeneo yao
wanamoishi.
Subscribe to:
Posts (Atom)